Utekaji Nyara wa Paul Edwin Overby, Jr.

Asia Kusini na Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 5

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa zitakazowezesha kumpata, kumuokoa, na kumrejesha Paul Edwin Overby, Jr. Mnamo katikati ya mwezi Mei, mwaka 2014, Overby, mwandishi Mmarekani, alitoweka mkoani Khost, Afuganistani, ambako alikuwa akifanya utafiti kwa ajili ya mradi wa kitabu. Kabla ya kutoweka kwake, Overby alidokeza kwamba alipanga kuvuka mpaka na kuingia Pakistani ili kuendeleza utafiti wake. Alionekana mara ya mwisho mjini Khost, nchini Afuganistani. Overby ana ugonjwa wa mfreji wa ndani wa sikio unaohitaji matibabu na dawa.

Skip to content