Shambulio la Kigaidi Dhidi ya Wamarekani nchini Bangladesh

Asia Kusini na Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 5

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu mauaji ya Avijit Roy na shambulio wakati huo huo la Rafida Bonya Ahmed kwenye eneo la Dhaka, nchini Bangladeshi.

Mnamo tarehe 26 mwezi Februari, mwaka 2015, raia wa Marekani waliozaliwa Bangladeshi na wanandoa Roy na Ahmed walikuwa wakitembelea Dhaka kuhudhuria maonyesho ya vitabu wakati waliposhambuliwa na wavamizi wasiojulikana wenye mapanga. Roy alikatwakatwa hadi kifo. Ahmed alinusurika akiwa na majeraha mabaya, kikiwapo kidole gumba kilichokatika kabisa na vidonda vingi vya kichwani.

Kama mwandishi, mwanablogu, na mwanaharakati, Roy alipinga ukereketwa wa kidini nchini Bangladeshi kwa kutetea uhuru wa kujieleza. Aliratibu maandamano ya kimataifa ili kuhamasisha kuhusu hali mbaya ya wanablogu wakanamungu waliofungwa gerezani nchini Bangladeshi na alikuwa mhakiki maarufu wa ugandamizaji wa kijamii. Alilengwa na kuuliwa kwa kuzungumzia wazi mambo aliyoamini na uanaharakati wake.

Ansarullah Bangla Team (ABT), kundi la kigaidi la Bangladeshi, lilidai kuhusika na shambulio hilo. ABT hujaribu kuwafunza vijana itikadi kali ili kuua wale inaowaona kama wapinga Uislamu. Muda mfupi baadaye, kiongozi wa al-Qa’ida Kwenye Bara Dogo la Indian (AQIS) marehemu Asim Umar, alichapisha video iliyosambazwa sana ikidai kuwa wafuasi wa AQIS, wakiwamo wale ambao bado hawajakamatwa, walihusika na shambulio hilo dhidi ya Roy na Ahmed.

Mnamo tarehe mosi, mwezi Julai, mwaka 2016, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilitaja AQIS kama Shirika la Kigaidi la Kigeni chini ya kifungu 219 cha Sheria ya Uhamiaji na Uraia, kama ilivyorekebishwa. Hapo awali, mnamo tarehe 30 mwezi Juni, mwaka 2016, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilitaja AQIS kama Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Matokeo ya kutajwa huku, miongoni mwa matokeo mengine, ni kwamba mali yote na maslahi ya AQIS katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na AQIS. Ni kosa la jinai kutoa kwa makusudi, au kujaribu au kula njama ya kutoa, msaada wa nyenzo au rasilimali kwa AQIS.

Waliohusika na shambulio hilo wanaaminika kuwa wako nchini Bangladeshi.

Skip to content