Kuhusu
Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu shambulio la bomu la mwaka 1993 dhidi ya majengo ya World Trade Center mjini New York. Mnamo tarehe 26 mwezi Februari, mwaka 1993, magaidi walilipua bomu la pauni 1,500 ndani ya lori kwenye maegesho chini ya majengo ya World Trade Center. Mlipuko huo uliwaua watu sita, ukawajeruhi wengine zaidi ya 1,000, na ukasababisha uharibifu wa mamia ya mamilioni ya dola.

Kundi la watu waliohusishwa na al-Qa’ida (AQ), wakiwamo Abdul Rahman Yasin na Ramzi Yousef, walipanga shambulio hilo. Khalid Sheikh Mohammed, mwanachama wa cheo cha juu wa AQ na mjomba wa Yousef, alitoa ufadhili kwa shambulio hilo. Wahalifu hao walitumaini bomu hilo lingaliangusha mnara mmoja, huku vifusi kutoka kwa maporomoka hayo vikiugonga na kuuangusha mnara wa pili. Watu sita waliopanga shambulio hilo, akiwamo mwanzilishi mwamba Ramzi Yousef, walikamatwa, wakashtakiwa na wakapatikana na hatia, na kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani. Mla njama wa saba, Abdul Rahman Yasin, angali mtoro.
