Kuhusu
Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu shambulio la bomu dhidi ya Klabu ya USO mjini Naples, Italia. Mnamo tarehe 14 mwezi Aprili, mwaka 1988, bomu la gari lililipuka kwenye sehemu ya mbele ya eneo, likawaua watu watano, akiwamo mwanajeshi wa kike wa Marekani, na kuwajeruhi watu wengine 15, wakiwamo wanajeshi wanne wa Marekani.

Junzō Okudaira, mwanachama wa kundi la kigaidi la Jeshi Jekundu la Japani, alifunguliwa rasmi mashtaka nchini Marekani mnamo tarehe 9 mwezi Aprili, mwaka 1993, kwa shambulio hilo la Klabu ya USO. Okudaira pia ni mtuhumiwa katika shambulio la bomu la kutegwa ndani ya gari na shambulio la kombora mnamo mwezi Juni, mwaka 1987 dhidi ya Ubalozi wa Marekani mjini Roma.
