Shambulio la Bomu Dhidi ya Chuo Kikuu cha Hebrew University

Mashariki ya Karibu - Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 5

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu shambulio la bomu la mnamo tarehe 31, mwezi Julai, mwaka 2002 dhidi ya Chuo Kikuu cha Kiebrania mjini Yerusalemu. Watu tisa, wakiwamo Wamarekani watano, waliuliwa na wengine 85 walijeruhiwa wakati bomu lililipuka ndani ya mgahawa wa Chuo Kikuu cha Kiebrania. Washambuliaji hao walitekeleza maagizo kutoka kwa viongozi wa kundi la kigaidi la Hamas.

Skip to content