Shambulio Dhidi ya Watalii Kwenye Mbuga ya Bwindi Park, Uganda

Afrika - Chini ya Jangwa la Sahara

Tuzo

Hadi dola milioni 5

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu shambulio dhidi ya watalii kwenye Mbuga ya Bwindi, Uganda, uliofanyika mnamo mwaka 1999.

Mnamo tarehe mosi, mwezi Machi, mwaka 1999, wanachama wa kundi la Jeshi la Ukombozi wa Rwanda (ALIR) waliwashambulia watalii wasiokuwa na silaha na waelekezi wao katika mbuga ya wanyama ya Bwindi Impenetrable National Park nchini Uganda. Kikundi hiki cha kitalii kilishambuliwa, kikatekwa nyara, na kikalazimishwa kutembea kwa miguu kikielekea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mganda mmoja, Paul Ross Wagaba, aliteketezwa akiwa hai. Wahanga wanane wa shambulio hilo, wakiwamo Wamarekani Susan Miller na Robert Haubner, walipigwa hadi kifo.

Barua iliyoandikwa kwa mkono ilipewa manusura wa shambulio hilo na kiongozi wa kundi hilo, ikisema kuwa shambulio hilo lilinuiwa kutuma ujumbe kwa Marekani na mataifa mengine ili yakome kuiunga mkono serikali ya Rwanda.

Skip to content