Kuhusu
Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni moja kwa taarifa kuhusu shambulio la tarehe 12 mwezi Januari, mwaka 2007 kwa makombora ya kurushwa kwa roketi dhidi ya Ubalozi wa Marekani jijini Athens, nchini Ugiriki. Kundi linalodai kuhusika, Mapambano ya Mapinduzi, linaaminika kuwa chipukizi la kundi la kigaidi la Ugiriki, 17 Novemba.
