Seher Demir Sen

Ulaya na Eurasia

Tuzo

Hadi dola milioni 3

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tatu kwa taarifa kumhusu Seher Demir Sen, anayejulikana pia kama Munever Koz or Alba, kiongozi muhimu katika Chama/Umoja wa Kimapinduzi wa Ukombozi wa Watu (DHKP/C), iliyotajwa na Marekani kuwa Shirika la Kigaidi la Kigeni. Shirika la DHKP/C limefanya mashambulio dhidi ya maslahi ya Marekani nchini Uturuki.

Sen alijiunga na shirika la Devrimci Sol (Dev Sol) mnamo mwaka 1980 na akabakia mwanachama hadi mwaka 1994 alipojiunga na DHKP/C baada ya Dev Sol kugawanyika. Alipanda ngazi hadi kufikia nafasi ya juu ya uongozi katika DHKP/C nchini Ugiriki, akiripotiwa kutumika kama mkuu wa ofisi ya kundi hilo jijini Athens. Sen ni mwanachama wa Kamati Kuu ya DHKP/C, iliyo chombo cha juu zaidi cha maamuzi cha kundi hilo.

Skip to content