Mauaji ya Maofisa wa Ubalozi Mdogo

Asia Kusini na Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 5

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu mauaji ya mwaka 1995 ya wafanyakazi wawili wa Ubalozi Mdogo wa Marekani mjini Karachi, Pakistani. Mnamo tarehe 8 mwezi Machi, mwaka 1995, gari jeupe lilikuwa limewabeba wafanyakazi wa Ubalozi Mdogo wa Marekani wakati ambapo teksi ya manjano ilipinda ghafla mbele yake kwenye njia panda yenye shughuli nyingi na kulilazimisha kusimama. Basi nalo gari jingine likalizuia hilo jeupe lisiweze kusogea. Magaidi waliofunika nyuso zao na wenye bunduki za kiatomatiki walilifyatulia risasi gari hilo jeupe na kuwaua wawili wa wafanyakazi wa ubalozi mdogo na kumjeruhi mwingine.

Skip to content