Mashambulio ya Mabomu Dhidi ya Eneo la Makazi Mjini Riyadh

Mashariki ya Karibu - Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 5

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kuhusu mashambulio ya mabomu kwenye eneo la makazi ya mwaka 2003 mji mkuu wa Saudia. Mnamo tarehe 12 mwezi Mei, mwaka 2003, angalau wavamizi 15 walishambulia maeneo matatu ya makazi jijini Riyadh. Baada ya kuvuja vizuizi vya usalama vyenye walinzi, washambuliaji hao walilipua mabomu ya gari kwenye maeneo hayo, wakawaua watu 35, wakiwamo Wamarekani tisa, na kuwajeruhi wengine karibu 200. Majengo yaliyolengwa yalikuwa yamewaajiri na kuwapa makao watu wengi kutoka mataifa ya Ulaya Magharibi, kwa mahususi raia wa Marekani na Uingereza. Al-Qa’ida ilipanga na kuratibu shambulio hilo.

Skip to content