Kuhusu
Tuzo kwa Mahakama inatoa kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kumhusu Malik Abou Abdelkarim, anayejulikana pia kama Abd al-Karim au Abu Abd al-Karim al-Tariqi. Abdelkarim ni kiongozi mwandamizi wa kikosi cha wapiganaji ndani ya kundi la al-Qa’ida Kwenye Maghreb ya Kiislamu (AQIM), lililotajwa na Marekani kuwa Shirika la Kigaidi la Kigeni.
Chini ya uongozi wa Abdelkarim, kikosi chake kilipata silaha na kutekeleza visa vya utekaji nyara na mashambulio madogo ya kigaidi kote Afrika Kaskazini na Magharibi. Inasemekana Abdelkarim alihusika na mauaji ya mateka mzee wa Kifaransa nchini Nijeri mnamo mwezi Julai, mwaka 2010. Shambulio la mwezi Juni, mwaka 2010 lililotekelezwa na kikosi cha Abdelkarim liliishia na mauaji ya askari polisi 11 wa Aljeria.
