Kuhusu
Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kumhusu Faker Ben Abdelaziz Boussora, anayejulikana pia kama Abu Yusif al-Tunisi au Fakeroun. Boussoura ni jasusi aliyefunzwa na al-Qaida (AQ) aliyetangaza nia za kuwa mlipuaji bomu wa kujitoa mhanga. Ana uhusiano mpana na Waislamu wenye misimamo na itikadi kali na ni mshirika wa mshukiwa wa ugaidi wa AQ, raia wa Tunisia, Abderraouf Jdey. Boussora aliondoka Tunisia, alikozaliwa, mnamo mwaka 1988 na akahamia Ufaransa. Aliondoka Ufaransa mnamo mwaka 1991 na kuhamia Montreal, Kanada, akisafiri kwenda na kurudi kutoka Kanada hadi Tunisia mara nyingi wakati wa miaka ya tisini 1990. Boussora alipata uraia wa Kanada mnamo mwaka 1999. Mwaka huo huo, Boussora aliondoka Kanada kwenda Afuganistani, ambako alipata mafunzo ya kigaidi kutoka AQ. Boussora baadaye alirejea Kanada. Hajulikani aliko wakati huu. Mamlaka zingali na wasiwasi kwamba huenda Boussora akarejea Kanada au Marekani ili kupanga au kushiriki katika shambulio la kigaidi. Labda anaugua ugonjwa mbaya na huenda afya yake ni mbaya sana, na hiyo kusababisha kupoteza uzito na sura yake kubadilika.
