Kuhusu
Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kumhusu Ali Saed bin Ali el-Hoorie, anayejulikana pia kama Ali Saed bin Ali al-Houri. El-Hoorie, anayedaiwa kuwa mwanachama wa shirika la kigaidi la Saudi Hizballah, anasakwa kwa jukumu lake katika shambulio la bomu la mwaka 1996 kwenye jumba la Khobar Towers karibu na Dhahran, Saudia.
Mnamo tarehe 25 mwezi Juni, mwaka 1996, wanachama wa Saudi Hizballah walilipua lori la kubebea mafuta lililokuwa na vilipuzi vya plastiki kwenye eneo la maegesho la Khobar Towers, jumba la makazi lililotumiwa kama makao ya wanajeshi wa Marekani. Mlipuko huo nusura uliharibu kabisa jengo lililokuwa karibu, ukawaua wanajeshi 19 wa Marekani na raia mmoja wa Saudia na kujeruhi mamia ya watu wengine kutoka mataifa mbalimbali.
Mnamo tarehe 21 mwezi Juni, mwaka 2001, jopo kuu la mahakama ya serikali kuu ya Marekani lilimfungulia rasmi mashtaka el-Hoorie na watu wengine 13 waliohusishwa na shambulio hilo.
Mnamo tarehe 12 mwezi Oktoba, mwaka 2001, Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Marekani ilimtaja el-Hoorie kuwa Gaidi wa Kimataifa Mwenye Sifa Maalumu kuambatana na Amri ya Rais 13224, kama ilivyorekebishwa. Matokeo ya kutajwa huku, miongoni mwa matokeo mengine, ni kwamba mali yote na maslahi ya el-Hoorie katika mali, vyote vilivyoko chini ya mamlaka ya Marekani vimezuiwa, na watu wa Marekani kwa jumla wamekatazwa kushiriki kwenye miamala yoyote na el-Hoorie. Yupo kwenye Orodha ya Magaidi Wanaosakwa Zaidi ya Shirika la FBI.
