Abderraouf Ben Habib Jdey

Amerika Kaskazini na Kusini | Asia Kusini na Kati | Mashariki ya Karibu - Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati

Tuzo

Hadi dola milioni 5

Fanya jukumu lako.

Kuhusu

Tuzo kwa Mahakama inaahidi kutoa tuzo ya hadi dola milioni tano kwa taarifa kumhusu Abderraouf Ben Habib Jdey, anayejulikana pia kama Farouq al-Tunisi. Jdey amehusishwa kwa karibu na majasusi wa al-Qa’ida (AQ) na amehusika katika mipango ya kuteka nyara ndege na shughuli nyingine za kigaidi. Jdey ni mshirika wa gaidi mshukiwa Faker Ben Abdelaziz Boussora, na huenda wawili hao wamesafiri pamoja.

Jdey alizaliwa Tunisia mnamo mwaka 1965. Alihamia mjini Montreal, Kanada mnamo mwaka 1991 na akawa raia wa Kanada mnamo mwaka 1995. Mnamo mwaka 1999, Jdey aliondoka Kanada kuelekea Afuganistani, ambapo alipata mafunzo ya kigaidi na uzoefu wa vita. Alipigana vita dhidi ya Muungano wa Kaskazini mwa Afuganistani na akaandika barua akieleza nia yake ya kuwa mfiadini wa jihad. Wakati huu pia alionekana kwenye video ya kifo cha kishahidi iliyopatikana katika nyumba ya kiongozi wa AQ mnamo mwaka 2001.

Jdey alirejea eneo la Montreal mnamo mwaka 2001. Baada ya kushauriana na wengine wenye itikadi kali kuhusu kujiiunga na jihad, aliondoka Kanada. Mamlaka ina hofu kwamba huenda akarejea Kanada au Marekani kupanga au kushiriki katika shambulio.

Skip to content